Sunday, 17 November 2013

ANGALIA PICHA YA MWANAMKE ALIYEKATWA MGUU NA MUWE WAKE TARIME

Hali ya wanawake inazidi kuwa mbaya ndani ya nchi yao TANZANIA inayosifiwa kuwa ni Kisiwa cha Amani (Amani kwa wanaume) Tukio hili lilitokea mapema mwezi wa nane mwaka huu Kijiji cha Nyantira Tarime Mara. Katika mazungumzo yake huyu binti alisema kwamba anatamani sana kurudi nyumbani kwa wazazi wake, tatizo ni kwamba kwa kuwa alilipiwa MAHARI na mume wake (aliyemkata panga mguu na kuutoa) hawezi kurudi kwao , wala mama yake hawezi kumkubalia arudi kwao ni mpaka baba yake aje atoe ruhusa ya yeye kurudi nyumbani au abaki kwa mume muuaji avumilie-MFUMO DUME UMEKAMATA MIZIZI (mbayaaaaa, sanaaaa. anajisemeaga Mch Rwakatare)

MBWANA SAMATA KUSHINDANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA



Shirikisho la kandanda barani Afrika CAF limetangaza majina ya wachezaji wa kiafrika watakaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2013 na Mchezaji bora wa Afrika anayechezea vilabu vya ndani ya Afrika mwaka 2013.
Katika majina hayo yapo majina mawili ya wachezaji wanaotoka Afrika Mashariki ambao ni Victor Wanyama raia wa Kenya anachezea Southampton FC ya England ambaye ni miongoni mwa wachezaji 25 watakaowania tuzo ya Mchezaji bora wa Afrika, huku Mbwana Samatta raia wa Tanzania anayechezea klabu ya TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo yeye ameteuliwa kuwania tuzo ya Mchezaji bora wa Afrika anayechezea timu za Afrika.
Wachezaji 25 watawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika na 21 Mchezaji bora wa Afrika anachezea timu za ndani ya Afrika.
Washindi wa tuzo hizo wanatarajiwa kutangazwa Januari 9, mwaka 2014 mjini Lagos nchini Nigeria.
Orodha kamili ya wachezaji waliotangazwa na CAF na timu wanazotoka hii hapa chini.

Mchezaji wa bora wa CAF Afrika

1. Ahmed Musa - Nigeria - CSKA Moscow
2. Asamoah Gyan - Ghana - Al Ain
3.Dame N'Doye - Senegal - Locomotiv Moscow
4. Didier Drogba - Cote d'Ivoire - Galatasaray
5. Emmanuel Emenike - Nigeria - Fenerbahce
6. Islam Slimani - Algeria - Sporting Lisbon
7. John Mikel Obi - Nigeria - Chelsea
8. Jonathan Pitroipa - Burkina Faso - Stade Rennais
9. Kévin Constant - Guinea - AC Milan
10. Kwadwo Asamoah - Ghana - Juventus
11. Luís Carlos Almada Soares (platini) - Cape Verde - AC Omonia
12. Mehdi Benattia - Morocco - AS Roma
13. Mohamed Aboutrika - Egypt - Al Ahly
14. Mohamed Salah - Egypt - Basel FC
15. Nicolas Nkoulou - Cameroon - Marseille
16. Pierre-Emerick Aubameyang - Gabon - Borussia Dortmund
17. Ryan Isaac Mendes da Graça - Cape Verde - Lille
18. Saladin Said - Ethiopia - Wadi Degla FC

Wednesday, 13 November 2013

BARUA YA POLISI WA UINGEREZA KWA TANZANIA KUMTAFUTA GODBLESS LEMA KWA KOSA LA KUMBAKA FLORA LYIMO..!






Hii ni barua ya polisi wa uingereza waliyoandikia polisi ya tanzania wakimtafuta lema akamatwe kwa kosa la ubakaji.

maelezo ya ziada ambayo uingereza walihitaji kutoka polisi ya Tanzania, ni haya hapa chini.

Ushahidi wa mbunge Godbless Lema kumbaka flora lyimo wazidi kubainika

Taarifa za kweli kuhusu mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema kumbaka mwanadada Flora Lyimo tarehe 8.8.2012 nchini Uingereza wakati wa ufunguzi wa tawi la chadema nchini humo umezidi kubainika.

Tarehe 2 -3, january 2013 akiwa tanzania, Flora aliwasilisha barua ya polisi wa uingereza kwa polisi kituo cha Moshi mkoani kilimanjaro na kufunguliwa jalada no.MOS/RB/17127/12.

Aidha tarehe 13/12/2012 Afisa upelelezi DC William Hughes wa kitengo cha uhalifu jeshi la polisi la uingereza kituo cha 4-6 shepherdess walk N17LF alifika ubalozi wa Tanzania nchini uingereza ili kujua pamoja na mambo mengine, 
-Taarifa sahihi za GODBLESS LEMA 
-Anuani yake 
-Barua pepe 

Ushauri kutoka mamlaka za Tanzania juu ya mikakati mizuri ya kushughulikia kesi hiyo ambayo inamuhusisha kiongozi wa chama kikubwa cha siasa na 
-Wasifu wake. 

Mbali na tukio hilo kuripotiwa ubalozini, vyanzo mbalimbali vya habari ikiwa ni pamoja na Gazeti la changamoto la tanzania toleo namba 348 la tarehe 18- 24 desemba 2012 lilichapisha taarifa ya tukio hilo kwenye ukurasa wake wa mbele.kwa kichwa cha habari "POLISI UINGEREZA WAMSAKA LEMA", Pia blog ya global publishers ya nchini tanzania katika report zake za tarehe 14 mei 2013 iliandika habari hiyo kwa kichwa cha habari "MREMBO;MBUNGE AMENIBAKA" Ambapo mrembo huyo (flora) alieleza alivyochaniwa na kufanyiwa kitendo hicho. alieleza kuwa lema alikuwa amemsindikiza mpaka nyumbani na walipofika LEMA aliomba aonyeshwe sehemu ya kujisaidia haja ndogo ndipo alipomvamia Flora na kumchania nguo na kutekeleza azma yake hiyo ovu.

Flora amekuwa akionekana katika shughuli mbalimbali za kijamii lakini ana wasiwasi kuwa anaweza kufanyiwa unyama na LEMA wakati akiwa Tanzania kwa sababu anasema anamfahamu lema pia kuwa ana asili ya ujambazi.

kiambatisho ni barua ya polisi wa kimataifa interpol kumweleza kuwa uchunguzi wa kesi yake unaendelea.

Chanzo:Jamii Forums

"Diamond Platnumz siwezi kumlinganisha hata kidogo na Alikiba..." MASOUD....!SOMA ZAIDI HAPA!

Wiki iliyopita katika kipindi cha Mkasi ambacho hurushwa kupitia EATV na kuendeshwa na mtangazaji Salama Jabir, mgeni alikuwa Masoud Masoud, mtangazaji mahiri wa muda mrefu ambaye ni miongoni mwa watangazaji wa Radio wanaoheshimika sana Tanzania kutokana na upeo mkubwa alionao na kufahamu mambo 
mengi.



Masoud Masoud  
Moja ya swali aliloulizwa ni “Labda kuna tamasha wewe ndio muandaaji au wamekwambia uchague mwanamuziki ambaye ataenda kuburudisha kwenye hilo tamasha Tanzania utamchagua mwanamuziki gani?”

Masoud ambaye anasifa ya kuongea kwa uwazi bila kupindisha maneno alimtaja Alikiba kuwa ndiye msanii pekee wa bongo fleva anayemkubali kuliko mwingine yeyote.

“Mimi wa kwanza nitakayempendekeza aaah nani huyu, nampenda sana katika wasanii wote wa bongo fleva, Alikiba, Alikiba nampenda sana. Alikiba kama umemsikiliza, Rhyme zake zile katikati ya zile bars anavyoimba ni mwanamuziki kama angekuwa nje ya nchi asingekamatika. Angepata producer mzuri wa kumfahamisha nini cha kuimba beat gani atumie, Alikiba yuko juu sana.” Alijibu Masoud

Aliendelea na kuongeza kuwa Diamond anaweza kuwa anafanya vizuri sokoni lakini hawezi kumfikia hata kidogo Kiba katika uimbaji.

“Nyota imeng’aa kwa Diamond Platnumz lakini Diamond Platnumz siwezi kumlinganisha hata kidogo na Alikiba, kwenye kuuza huwezi kumlaumu anaweza kuwa Diamond akauza sana au akampandisha na si Tanzania tu, hata Hollywood wanafanya hivyo hata CBS wanafanya hivyo, hata US music industry wanfanya hivyo. Sasa mpaka wakiwepo watu wataalam wanaoweza kusema huyu anaimba sawa huyu haimbi sawa lakini kwenye mauzo hakuna mtu anajali hilo.”

HAYA NDIO MAISHA...!LADY JAYDEE 'ANACONDA' SASA YUPO MBIONI KUFUNGUA RADIO STATION YAKE.....!!


Nimeshangaa sana baada ya kuona AWARDS mbalimbali alizojinyakulia LADY JAYDEE tokea aanze muziki apa bongo mwaka 2000 hadi sasa 2013,tokea mwaka huo(2000) aanze muziki alibahatika kujinyakulia tunzo na hadi leo hii hajawahi kukosa tunzo ukijumlisha na zile alizopata Uganda kama mara nne au tano.

Hivi,tokea aanze muziki mwaka huo JIDE hajawahi kuchuja hadi leo hii bado yupo juu kimuziki hata kimaisha,kumbuka ni miaka kumi na tatu (13) sasa.Ki ukweli huyu msanii anahitaji heshima ya kipekee apa bongo na nchi za jirani pia.Hiki kitu sio cha kawaida kabisa kuwahi kutokea apa bongo.


Achilia mbali mafanikio aliyoyapata ya kujenga jumba la kifahari,kumiliki mgahawa wa kisasa (NYUMBANI LOUNGE),kumiliki band ya music,kufungua STUDIO YA MUZIKI,na hivi karibuni yupo njiani kufungua RADIO STATION yake binafsi,can u imagine???,kufungua radio station sio kitu cha kawaida hata kidog especially kwa wasanii wetu wa apa bongo.Kwa sasa HAKUNA msanii yeyote awe wa kike au wa kiume mwenye ubavu wa kushindana na huyu bidada,SHE IS THE NUMBER ONE.

Kama ulikuwa hujui huyu ndiyo KOMANDO na huu ndiyo UCHAWI ambao msanii yeyote wa bongo mwingine hajaweza kufanya..!!

PROFESA LIPUMBA AENDA KUIFARIJI FAMILIA YA DR MVUNGI

PROFESA LIPUMBA AKIMPA POLE MKE WA MAREHEMU DR MVUNGI
 


PROFESA LIPUMBA AKISAINI KITABU CHA RAMBI RAMBI

Monday, 11 November 2013

DIAMOND AFUNGUKA JUU YA YEYE KUMUOA WEMA SEPETU...

Rais wa Wasafi Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond’, juzikati alifunguka kuwa kwenye maisha yake ya ndoa atakayoingia siku chache zijazo, aliyekuwa mchumba wake wakamwagana na kurejeana hivi karibuni, Wema Sepetu asitegemee kuolewa naye. Diamond ambaye ni staa wa Bongo Fleva aliyasema hayo mbele ya paparazi wetu Novemba 7, mwaka huu jijini Dar kufuatia kuulizwa anamchagua nani wa kumuoa kati ya Wema Sepetu na mchumba wake wa sasa, Penniel Mungilwa ‘Penny’.

Swali kwa Diamond liliibuka baada ya kuzagaa kwa tetesi kwenye mitandao ya kijamii kwamba yu mbioni kumvisha pete ya uchumba mmoja wa mademu zake.
Swali hilo lilimfanya Diamond afunguke kwa kusema kwamba anachokijua yeye na ambacho kipo kwenye mikakati yake, mke wake mtarajiwa ni Penny. “Najua wengi wanahisi mimi ninaweza kuoa mwanamke zaidi ya mmoja kutokana na dini yangu kuruhusu lakini jambo hilo mimi silifikirii hata kidogo kwa kuwa kwenye maisha yangu nilishapanga nitaoa mke mmoja tu,” alisema Diamond. Akaendelea: “Watu wanasema mengi juu yangu na Wema, wengi wao hawajui nafsi yangu inataka mwanamke yupi, ninachoweza kusema na watu wakasikia na kunielewa basi wajue kwamba Penny ndiye mke wangu, Wema asitegemee kuolewa na mimi.” Diamond alikwenda mbele zaidi kwa kumwanika Penny kwamba ana sifa ya kuwa mke kwani ni mvumilivu sana na anaonesha upendo wa dhati kwake. “Kwa maana hii basi hakuna mwanamke mwenye jina  kubwa wala sura nzuri zaidi ya Penny ninayeweza kumwita mke wangu. Najua kila mtu ana namna yake ya kuchagua ampendaye, ndiyo maana utaona watu wanasema hili mara lile, lakini hawajui nafsi yangu inataka mwanamke wa aina gani,” alisema Diamond na kuongeza: Kama kuna demu anayejipa matumaini hayo basi asitegemee hata siku moja kwa sababu kuoa kwangu kutazingatia mke mwema na si bora mke, Penny pekee ndiye mwenye sifa za kuwa mke wangu,” alisema Diamond. Juzi Ijumaa Wikienda lilimpigia simu Penny ili kutaka kupata maoni yake kuhusu tamko la Diamond, lakini muda mrefu simu hiyo ilikuwa ikiita bila kupokelewa. Baada ya kumkosa Penny, Ijumaa Wikienda lilimtwangia simu Wema, naye kama Penny, simu yake iliita mara kadhaa lakini haikupokelewa
Facebook Blogger Plugin by JustNaira.com | Get Widget

Saturday, 9 November 2013

HATIMAYE MAMA DIAMOND AZUNGUMZIA PENZI JIPYA LA WEMA SEPETU KWA DIAMOND, UNAJUA KASEMA NINI? SOMA HAPA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6LFcmL5SHgtI1IChyphenhyphenN6NPO0ki72N3qkZHUOZWVMCUCN4I7vl5TAJfJ_-eadOXZ5SbftJNbBDbZhkXN7ca8seHUwh4WbwvoPSjXwvUOL8fGzlzsFIFbQga1I6Yrai20l2AMXH50CHXSfY/s640/4.jpegMsanii wa ngoma ya Number One, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kasim ‘Sandra’ ameingilia kati penzi lililofufuka upya kati ya mwanaye na staa wa filamu za Kibongo, Wema Sepetu.
Habari za chini ya kapeti zilitonya kuwa baada ya kuambiwa na kuoneshwa picha za Diamond akiwa kimahaba na Wema alikuja juu akidai kuwa hamtaki Wema kwa kuwa anamkubali zaidi Penniel Mungilwa ‘Penny’.
Akizungumza akiwa  nyumbani kwake Sinza-Mori jijini Dar wikiendi iliyopita, bi’mkubwa huyo alisema kuwa kwa sasa hafahamu chochote kuhusu Diamond kurudiana na Wema zaidi ya kusikia kwa watu na kuona picha katika mitandao ya kijamii.
“Kuhusu Nasibu (Diamond) kurudiana na Wema, nasikia tu na kuoneshwa picha namsubiri Nasibu arudi kisha nikae naye ndipo nitatoa tamko,” alisema mzazi huyo.
Mapaparazi wa Ijumaa Wikienda kadiri walivyozidi kumchimba mama mkwe huyo wa Wema ni jinsi gani anavyojisikia kuhusu tabia ya kubadilisha wanawake kama nguo, ikizingatiwa yeye ni mzazi haoni kama mwanaye anamfedhehesha alisema kuwa hayo ni maisha yake.
“Hayo ni maisha yake na mwenyewe kwa kuwa ameshazoea kuonekana katika magazeti kila wakati mi niongee nini wakati ndiyo maisha aliyojiwekea,” alimalizia kusema.

HUYU NDIYE MCHAWI ALIYEDONDOSHWA NA MAOMBI YA MAKOMANDOO WA VHM ALFAJIRI

Makomandoo wa VHM wakiwa katika Operation ya kusambaratisha kazi za shetani afajiri baada ya maombi mazito mama aliyekuwa na tumbo kubwa akidhaniwa ni mjamzito kumbe hakuwa na mimba yoyote. Baada ya maombi mazito chini ya usimamizi wa makomandoo ya Yesu kupitia Voice of Hope Ministry  alijikuta akitapika meno ya mbwa, nywele na vitu visivyojulikana. Siku chache

WATACHOMOKA KWELI

WAUAJI WA UNITED KESHO

Mesut Ozil

TEAM NEWS: WHO IS FIT


Matchday Show - Manchester United v Arsenal

ARSENAL:Normally, Flamini and Walcott will join us in the session this morning. Wilshere will join in as well, so we will see how they are after the session today. 

UNITED: David Moyes will be hoping to have Michael Carrick, Jonny Evans and Rafael in contention after injuries ruled the trio out of the trip to San Sebastian. Marouane Fellaini will be available as the suspension for his red card at Estadio Anoeta, of course, only applies in Europe. Jack Wilshere was due for tests on the injured ankle that sidelined him for the Liverpool and Dortmund fixtures, but Arsene Wenger was more hopeful over the possibility of a return for Theo Walcott and Mathieu Flamini.

(Official Music Video) Nay wa Mitego ft. Neiba - Salam Zao

ANGALIA PICHA JUMA KASEJA AKISAINI MKATABA YANGA

 















Mlinda mlango nambari moja nchini Tanzania kwa kipindi kisichopungua miaka 10 mfululizo Juma Kaseja Juma jana majira ya saa 2 usiku alisaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Young Africans yenye makao yake Twiga/Jangwani kwa kipindi cha miaka miwili.
Usajili wa Juma Kaseja kujiunga na klabu ya Yanga unafuatia mapendekezo ya benchi la ufundi katika ripoti waliyoikabidhi kwa kamati ya mashindano kwa ajili ya kuboresha kikosi






Juma Kaseja akisani mkataba wa kuicheza Yanga kwa miaka miwili mbele ya mwenyekiti wa kamati ya mashindano Bin Klebl


KASEJA APATA ZALI

Kipa Juma Kaseja amesaini mkataba wa kuichezea Yanga rasmi, mkataba huo umesainiwa jana Ijumaa na ataanza kuitumikia timu hiyo katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Kaseja amesaini kwa dau la Sh milioni 40.

NIPO TAYARI KUCHANGIA PENZI LA DIAMOND PLATINUMZ NA WEMA SEPETU: VJ PENNY

Mtangazaji wa kituo cha televisheni cha DTV, Peniela Mwingilwa ‘Penny’, ambaye ni mpenzi wa mkali wa Bongo Fleva Diamond Platinumz amesema yupo tayari kuchangia mapenzi na msichana mwingine yeyote ambaye atachukuliwa na mwanaume huyo anayempenda.

Penny katika Penny na Wema.

Penny ambaye ni chaguo la mama mzazi wa staa huyo wa kibao cha My Number One, aliiambia Globalpublishers  maneno hayo, yanayotafsiriwa kama yupo tayari kuchangia mapenzi na hasimu wake, Wema Sepetu ambaye ni Miss Tanzania 2006n na muigizaji wa filamu Swahiliwood

Friday, 8 November 2013

MAITI YAKUTWA NA KETE 600 ZA DAWA ZA KULEVYA


 Kete inayosadikika kumuua kijana huyo baada ya kupasukia tumboni.

WANAFUNZI WAWILI WA CBE WAPATA AJALI YA PIKIPIKI NA KUFARIKI MKOANI DODOMA


 Baadhi ya watu wakiisogeza miili ya Wanafunzi wa CBE Dodoma  walikufa kutokana na kuligonga tela la lori kwa nyuma kutokana na mwendo kasi huku lori hilo likiwa limetelekezwa zaidi ya wiki bila alama yoyote barabarani hapo.
Miili ya Marehemu Ramadhan Lesso na Gerge Lwandala inaonakana kabla ya kuondolewa katika kijiji cha Ihumwa barabara ya Morogoro Dodoma kabala ya kuondolewa na kuhifadhiwa katika chumba cha maiti hospital ya mkoa.

MTOTO AWA NA MIGUU MISITA

Tuesday, 9 July 2013

NI HUZUNI NA MAJONZI...ANGALIA PICHA ZA MAITI WALIOKUFA VURUGU ZA MISRI

WEMA SEPETU ASAKWA NA POLISI KWA KOSA LA KUMSHAMBULIA MENEJA WA HOTELI


DIVA wa filamu za Bongo ambaye pia ni Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu anasakwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Kawe, Dar es Salaam kwa tuhuma za kufanya fujo hotelini, kumtukana matusi ya nguoni na kumpiga makofi meneja wa hoteli hiyo, Godluck Kuyumbu. Songombingo hilo lilijiri saa tano usiku wa Jumatano iliyopita kwenye hoteli hiyo  iliyopo Kawe Beach, jijini Dar. 


Akizungumza na mwandishi wetu , meneja huyo alisema siku ya tukio majira ya saa nane mchana, Wema alifika kwenye mgahawa wa hoteli hiyo akiwa ameongozana na marafiki zake wapatao kumi.

Meneja huyo akaendelea kusema, ilipofika  saa tano usiku, Wema na marafiki zake  walionekana kuzidiwa na kilevi, wakaanza kufanya fujo kwa kupiga kelele, kitendo kilichowakera wateja waliokuwa katika mgahawa huo, wengi wakiwa ni Wazungu ambao waliondoka kutokana na fujo hizo. 


Aliongeza kuwa mmoja wa marafiki wa Wema ambaye ilidaiwa ni mpenzi wake, aliyejulikana kwa jina moja la D, alichukua glasi na kuipasua chini kwa makusudi huku meneja huyo akishuhudia.

Saturday, 22 June 2013

BOB JUNIOR APEWA KIPIGO KIKALI KARIAKOO BAADA YA KUIBA....NI KATIKA UTENGENEZAJI WA VIDEO YAKE MPYA YA KIMBIJI

MSANII MAARUFU WA BONGO FLEVA BOB JUNIOR AMEONYESHA KUDHAMIRIA KUWEZA KUTOA VIDEO KALI YA NYIMBO YAKE BAADA YA KUAMUO KUONYESHA VITENDO ZAIDI KWA KWENDA KARIAKOO NA KUFANYA VIDEO HAPO

Friday, 21 June 2013

WANAFUNZI UDSM WAPIGWA RISASI

Taarifa zilizotufikia zinaeleza kuwa wanafunzi wanne wa chuo kikuu cha Dar es salaam maarufu kwa jina la Chuo cha Mlimani wamevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo maeneo ya Yombo chuoni hapo.
Wanafunzi hao wanaosemekana kuwa ni wa mwaka wa nne na wa mwisho wa masomo walikuwa wanajisomea na kuandaa “Disertation” zao na kujikuta wakivamiwa na watu wanne na kuamuriwa watoe komputa zao na pochi za fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo, wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha,  na majambazi kuanza safari yao.

Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.

Chanzo kimeendelea kusema kuwa wanafunzi wa Chuo hicho waliwasiliana na uongozi ili kupata gari ili wamkimbize mwenzao Hospitalini, lakini ilipita takribani nusu saa hakuna majibu na ndipo walipoamua kujikusanya na kuamua kuwafuata viongozi. Kwa sasa mwanafunzi huyo amekimbizwa Hospitalini kupata matibabu zaidi na mpaka sasa hakuna taarifa yoyote iliyotoka, ingawa FULLSHANGWE inajitahidi kufuatilia suala hilo ili kupta taarifa zaidi na picha za tukio hilo.

HOUSEGIRL AJIRUSHA KUTOKA GHOROFANI

HAUSIGELI ambaye jina lake halikupatikana mara moja, nusura ajirushe chini kutoka ghorofa ya pili kwa kile kilichodaiwa kuwa aliogopa moto mkubwa uliozuka katika jengo la jirani na ghorofa alilokuwemo.
Tukio hilo lilijiri mapema asubuhi ya Juni 18, mwaka huu kwenye makutano ya Mtaa wa Nyamwezi na Mkunguni eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa majirani, baada ya kuona moto huo ulioambatana na wingu zito la moshi ukitoka kwenye jengo la jirani, hausigeli huyo alitoka dirishani na kutaka kujirusha chini bila kujali nguo zilizokuwa zikimvuka katika purukushani hiyo.
Alifanikiwa kukaa kwenye sehemu ya ukingo wa ghorofa hilo na kujiandaa kwa tukio la kwenda chini akiamini atakuwa amejiokoa na moto huo.
Hata hivyo, bosi wa hausigeli huyo alipoona zoezi hilo la hatari alitoa mkono dirishani na kumvutia ndani mfanyakazi wake huyo tukio ambalo lilijiri muda mfupi kabla ya Kikosi cha Zima Moto kufika na kufanikiwa kuuzima bila kujeruhi mtu.

HATARIII....PICHA ZA BINADAMU ALIYEJIGEUZA KUWA MBWA ZICHEKI HAPA

NAY WA MANZESE AMPIGISHA MLEGE DEMU WAKE

[clip_image002%255B5%255D.jpg]Ukitaka kutoka na mimi lazima ushushe mlege ukizingua hautoki na mimi? umekuja kwa mwana hih hop lazima utoke kihihhop hapa hakuna kuvaa kibongo fleva, alisikika akimwambia mpenzi wake.

Thursday, 20 June 2013

DEMU WA BALLOTELI AWA KIVUTIO UWANJANI BRAZIL

Mpenzi wa mshambuliaji wa timu ya taifa ya Italia Fanny Neguisha ameonekana kuwa moja ya vivutio kwenye michuano ya kombe la mabara inayoendelea huko nchini Brazil. Fanny amekuwa akihudhuria mechi zote za Italia na usikuwa kuamkia leo alikuwepo
uwanjani wakati Italia inacheza na Japan huku akiwa amevalia jezi ya Italia.
Kwa wasiomfahamu wanaweza kudhania kuwa mwanamitindo huyo ni raia wa Italia kwa uzalendo aliouonyesha akiwa uwanjani lakini yeye ni raia wa Ubelgiji . Uwepo wa Fanny uwanjani unaonekana kumsaidia Super Mario ambaye alifunga moja ya mabao yaliyoisaidia  Italia kushinda 4-3.
Hivi karibuni Mrio alimvika mpenzi wake Fanny pete ya uchumba yenye thamani ya paundi laki moja baada ya tetesi kuwa zimesikika juu ya wawili hao kuachana kwenye mataa.

OFFICIAL VIDEO{MAJANGA by SNURA}

NEW[OFFICIAL] VIDEO.....snura Wa MAJANGA

Tuesday, 18 June 2013

SABABU ZA JESHI LA POLISI KUTUMIA NGUVU YA MABOMU JIJINI ARUSHA MUDA HUU


Jeshi la polisi limekipiga marufuku chama cha demokrasia na maendelo(CHADEMA)kufanya shughuli zozote za kuaga miili ya marehemu kwenye viwanja vya Soweto kwani zoezi la uchunguzi bado linaendelea kwenye viwanja hivyo .

Akizungumza ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas amesema kutokana na uchunguzi unaoendelea wa tukio la bomu kwenye viwanja hivyo imeonelea kuwa si busara kuweka mkusanyiko wa watu kwani kutaharibu upelelezi.


Kamanda Sabas amedai  kuwa  jeshi la polisi  liliwataka viongozi wa chama hicho kuwaeleza wafuasi wao mahali sahihi watakapoweza kufanyia shughuli hiyo lakini si kwenye viwanja hivyo.

Hali kwenye viwanja hivyo imekuwa ya pilika pilika tangu juzi kwa wafuasi wa chama hicho kujikusanya tokea asubuhi hadi jioni kwa madai ya kuomboleza ..

Hata hivyo viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo walikaidi agizo hilo na  kuanza  kujikusanya uwanjani hapo pamoja na wafuasi wa CHADEMA , hali iliyoleta  mvutano kati ya viongozi  wa jeshi la polisi na  wafuasi hao.

Wakati mabishano hayo yakiendelea, Askari Polisi mmoja  alijichanganya na kuingia katikati ya wafuasi wa Chadema pembeni mwa uwanja huo ambao walikua wanasubiri kujua utaratibu wa kuaga miili ya Marehemu waliolipuliwa na bomu June 15 2013.

BreakingNewzzzz...:Sugu apata ajali akiwa njiani kuelekea Arusha

 
..Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi amepata ajali hivi punde katika eneo la kasheki wilayani Hanan'g akielekea Arusha mjini.

Joseph Mbilinyi maaru Sugu alikuwa akielekea Arusha mjini kuungana na wabunge wengine ktk shughuli ya kuaga marehemu
waliolipukiwa na bomu kwenye mkutano wa Chadema, mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika ajali hiyo hakuna mtu yoyote amejeruhiwa, Mbunge huyo yuko salama, gari la Sugu limeharibiwa vibaya baada ya kugongana na basi la abiria.

MTANZANIA NANDO HATARINI KUTOLEWA BIG BROTHER ..KURA YAKO MUHIMU KUMUOKOA


Ni wiki tatu zimepita tukishuhudia Eviction shows tatu zilizowapa tiketi za kurudi makwao washiriki 6 mpaka sasa, na tumeshuhudia mshiriki wetu Feza Kessy akiponea kwenye tundu la sindano baada ya kura za wa Tanzania na wa Afrika kumuokoa, sasa ni zamu ya Nando ambaye yuko hatarini wiki hii.

Big Brother jana ametaja majina ya washiriki 7 ambao wako hatarini kutoka wiki hii na kati yao yupo kijana mpole, mtanashati, ‘handsome’ Nando anaeiwakilisha Tanzania, ikiwa ndio mara yake ya kwanza kupendekezwa .
Washiriki wengine walipigiwa kura nyingi kutoka wiki hii ni love birds Bolt na Betty, ambao hii si mara yao ya kwanza kupendekezwa baada ya kuponea chupuchupu kwa mara kadhaa.
Kenya wiki hii iko salama kwa mshiriki wao mmoja aliyesalia Annabel, japo kuwa alipendekezwa kutoka wiki hii lakini kilichomuokoa ni yeye kuwa mkuu wa nyumba ya Diamond, hivyo amepata favor ya kujiokoa mwenyewe na nafasi yake akampendekeza Motamma wa Botswana.

Kwa ujumla walioingia wiki hii ni Nando wa Tanzania, Natasha wa Malawi, Oneal wa Botswana, Motamma wa Botswana, Betty wa Ethiopia, Bolt wa Sierra Leon na Elikem wa Ghana.
Tanzania bado ina nafasi nzuri sababu washiriki wote wawili Nando na Feza wapo mjengoni na ndio maana unakila sababu ya kumpigia kura mara nyingi uwezavyo Nando ili aweze kubaki wiki hii. 

Washiriki wawili kati ya saba waliopendekezwa watapita kwenye mlango wa ‘EXIT’ mjengoni hapo Jumapili hii (June 23) wakati wa Eviction Show.

Monday, 17 June 2013

SINTAH AMTOLEA UVIVU OMMY DIMPOZ NA KUMPA LAKE LA ROHONI


Sinta ameandika haya yafuatayo katika website yake:

MDOMO UMEMPONZA HUYU KIJANA

"Daaah masikini akipata matako hulia mbwata, yaani nimesikitishwa na habari ya Ommy Dimpoz na kauli yake aliyotoa kwenye umma, hivi wewe Dimpozi unajua nini cha kuongea ktk public?? SMH usipende kuropoka ropoka tu hata kama wewe ukifa tutajuaje kwenye bank yako kuna kiasi gani acha kuongea kwasababu ya nyimbo tatu ,, Nainai, Badaye na Me n U, Angalia kijana na usiache mbachao kwa msala upitao sasa unajiliza nini katika radio na umeongea mwenyewe hivi hujui mdomo huumba na pia huponza kichwa??

sasa wewe unataka kuniambia u have invested na hutegemei show?? kumbuka sisi mashabiki wako ndio tumekuweka hapo juu na ku support music wako haya tukiacha kupenda nyimbo zako na ukakosa show itakuwaje??? umenizije sasa kumkejeli mwenzio tena kwenye kipaza sauti next time uliza nini cha kuongea ndio maana wenzenu wanakuwa na managers wa kuwa guide sio unaongea tu coz usikike. wenzio walionyamaza uliwaona mafala sio?? au ulitaka utoke kama hivi tukuongeleee cheap cheap fame.

kauli yako uko sahihi ila kwanini usingeiongelea ktk interviews zako kama ushauri kwa wasanii wenzio na ukaifanya ni big issue ktk msiba wa mwenzio??

nimekupa langu la roho kazi kwako sasa ukinichukia sijali, ukinipenda sawa coz naongea ukweli na wananchi waliokerwa wamenituma na sikuwepo ila wamerekodi wakaniambia CEO ifanyie kazi Ommy D katukwaza" says Sintah
Facebook Blogger Plugin by JustNaira.com | Get Widget

ASANTE KWA KUPATA HUDUMA ZETU,TUNAKUOMBA BOFYA LIKE KUUNGANA NASI FACEBOOK

No comments:

Post a Comment

page counter

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Naomba Maoni yako hapa

Scroll to top widget @Netoops Blog.blogspot.com