Saturday, 22 June 2013

BOB JUNIOR APEWA KIPIGO KIKALI KARIAKOO BAADA YA KUIBA....NI KATIKA UTENGENEZAJI WA VIDEO YAKE MPYA YA KIMBIJI

MSANII MAARUFU WA BONGO FLEVA BOB JUNIOR AMEONYESHA KUDHAMIRIA KUWEZA KUTOA VIDEO KALI YA NYIMBO YAKE BAADA YA KUAMUO KUONYESHA VITENDO ZAIDI KWA KWENDA KARIAKOO NA KUFANYA VIDEO HAPO

Friday, 21 June 2013

WANAFUNZI UDSM WAPIGWA RISASI

Taarifa zilizotufikia zinaeleza kuwa wanafunzi wanne wa chuo kikuu cha Dar es salaam maarufu kwa jina la Chuo cha Mlimani wamevamiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo maeneo ya Yombo chuoni hapo.
Wanafunzi hao wanaosemekana kuwa ni wa mwaka wa nne na wa mwisho wa masomo walikuwa wanajisomea na kuandaa “Disertation” zao na kujikuta wakivamiwa na watu wanne na kuamuriwa watoe komputa zao na pochi za fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo, wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha,  na majambazi kuanza safari yao.

Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.

Chanzo kimeendelea kusema kuwa wanafunzi wa Chuo hicho waliwasiliana na uongozi ili kupata gari ili wamkimbize mwenzao Hospitalini, lakini ilipita takribani nusu saa hakuna majibu na ndipo walipoamua kujikusanya na kuamua kuwafuata viongozi. Kwa sasa mwanafunzi huyo amekimbizwa Hospitalini kupata matibabu zaidi na mpaka sasa hakuna taarifa yoyote iliyotoka, ingawa FULLSHANGWE inajitahidi kufuatilia suala hilo ili kupta taarifa zaidi na picha za tukio hilo.

HOUSEGIRL AJIRUSHA KUTOKA GHOROFANI

HAUSIGELI ambaye jina lake halikupatikana mara moja, nusura ajirushe chini kutoka ghorofa ya pili kwa kile kilichodaiwa kuwa aliogopa moto mkubwa uliozuka katika jengo la jirani na ghorofa alilokuwemo.
Tukio hilo lilijiri mapema asubuhi ya Juni 18, mwaka huu kwenye makutano ya Mtaa wa Nyamwezi na Mkunguni eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa majirani, baada ya kuona moto huo ulioambatana na wingu zito la moshi ukitoka kwenye jengo la jirani, hausigeli huyo alitoka dirishani na kutaka kujirusha chini bila kujali nguo zilizokuwa zikimvuka katika purukushani hiyo.
Alifanikiwa kukaa kwenye sehemu ya ukingo wa ghorofa hilo na kujiandaa kwa tukio la kwenda chini akiamini atakuwa amejiokoa na moto huo.
Hata hivyo, bosi wa hausigeli huyo alipoona zoezi hilo la hatari alitoa mkono dirishani na kumvutia ndani mfanyakazi wake huyo tukio ambalo lilijiri muda mfupi kabla ya Kikosi cha Zima Moto kufika na kufanikiwa kuuzima bila kujeruhi mtu.

HATARIII....PICHA ZA BINADAMU ALIYEJIGEUZA KUWA MBWA ZICHEKI HAPA

NAY WA MANZESE AMPIGISHA MLEGE DEMU WAKE

[clip_image002%255B5%255D.jpg]Ukitaka kutoka na mimi lazima ushushe mlege ukizingua hautoki na mimi? umekuja kwa mwana hih hop lazima utoke kihihhop hapa hakuna kuvaa kibongo fleva, alisikika akimwambia mpenzi wake.

Thursday, 20 June 2013

DEMU WA BALLOTELI AWA KIVUTIO UWANJANI BRAZIL

Mpenzi wa mshambuliaji wa timu ya taifa ya Italia Fanny Neguisha ameonekana kuwa moja ya vivutio kwenye michuano ya kombe la mabara inayoendelea huko nchini Brazil. Fanny amekuwa akihudhuria mechi zote za Italia na usikuwa kuamkia leo alikuwepo
uwanjani wakati Italia inacheza na Japan huku akiwa amevalia jezi ya Italia.
Kwa wasiomfahamu wanaweza kudhania kuwa mwanamitindo huyo ni raia wa Italia kwa uzalendo aliouonyesha akiwa uwanjani lakini yeye ni raia wa Ubelgiji . Uwepo wa Fanny uwanjani unaonekana kumsaidia Super Mario ambaye alifunga moja ya mabao yaliyoisaidia  Italia kushinda 4-3.
Hivi karibuni Mrio alimvika mpenzi wake Fanny pete ya uchumba yenye thamani ya paundi laki moja baada ya tetesi kuwa zimesikika juu ya wawili hao kuachana kwenye mataa.

OFFICIAL VIDEO{MAJANGA by SNURA}

NEW[OFFICIAL] VIDEO.....snura Wa MAJANGA

Tuesday, 18 June 2013

SABABU ZA JESHI LA POLISI KUTUMIA NGUVU YA MABOMU JIJINI ARUSHA MUDA HUU


Jeshi la polisi limekipiga marufuku chama cha demokrasia na maendelo(CHADEMA)kufanya shughuli zozote za kuaga miili ya marehemu kwenye viwanja vya Soweto kwani zoezi la uchunguzi bado linaendelea kwenye viwanja hivyo .

Akizungumza ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas amesema kutokana na uchunguzi unaoendelea wa tukio la bomu kwenye viwanja hivyo imeonelea kuwa si busara kuweka mkusanyiko wa watu kwani kutaharibu upelelezi.


Kamanda Sabas amedai  kuwa  jeshi la polisi  liliwataka viongozi wa chama hicho kuwaeleza wafuasi wao mahali sahihi watakapoweza kufanyia shughuli hiyo lakini si kwenye viwanja hivyo.

Hali kwenye viwanja hivyo imekuwa ya pilika pilika tangu juzi kwa wafuasi wa chama hicho kujikusanya tokea asubuhi hadi jioni kwa madai ya kuomboleza ..

Hata hivyo viongozi wa chama cha demokrasia na maendeleo walikaidi agizo hilo na  kuanza  kujikusanya uwanjani hapo pamoja na wafuasi wa CHADEMA , hali iliyoleta  mvutano kati ya viongozi  wa jeshi la polisi na  wafuasi hao.

Wakati mabishano hayo yakiendelea, Askari Polisi mmoja  alijichanganya na kuingia katikati ya wafuasi wa Chadema pembeni mwa uwanja huo ambao walikua wanasubiri kujua utaratibu wa kuaga miili ya Marehemu waliolipuliwa na bomu June 15 2013.

BreakingNewzzzz...:Sugu apata ajali akiwa njiani kuelekea Arusha

 
..Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi amepata ajali hivi punde katika eneo la kasheki wilayani Hanan'g akielekea Arusha mjini.

Joseph Mbilinyi maaru Sugu alikuwa akielekea Arusha mjini kuungana na wabunge wengine ktk shughuli ya kuaga marehemu
waliolipukiwa na bomu kwenye mkutano wa Chadema, mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika ajali hiyo hakuna mtu yoyote amejeruhiwa, Mbunge huyo yuko salama, gari la Sugu limeharibiwa vibaya baada ya kugongana na basi la abiria.

MTANZANIA NANDO HATARINI KUTOLEWA BIG BROTHER ..KURA YAKO MUHIMU KUMUOKOA


Ni wiki tatu zimepita tukishuhudia Eviction shows tatu zilizowapa tiketi za kurudi makwao washiriki 6 mpaka sasa, na tumeshuhudia mshiriki wetu Feza Kessy akiponea kwenye tundu la sindano baada ya kura za wa Tanzania na wa Afrika kumuokoa, sasa ni zamu ya Nando ambaye yuko hatarini wiki hii.

Big Brother jana ametaja majina ya washiriki 7 ambao wako hatarini kutoka wiki hii na kati yao yupo kijana mpole, mtanashati, ‘handsome’ Nando anaeiwakilisha Tanzania, ikiwa ndio mara yake ya kwanza kupendekezwa .
Washiriki wengine walipigiwa kura nyingi kutoka wiki hii ni love birds Bolt na Betty, ambao hii si mara yao ya kwanza kupendekezwa baada ya kuponea chupuchupu kwa mara kadhaa.
Kenya wiki hii iko salama kwa mshiriki wao mmoja aliyesalia Annabel, japo kuwa alipendekezwa kutoka wiki hii lakini kilichomuokoa ni yeye kuwa mkuu wa nyumba ya Diamond, hivyo amepata favor ya kujiokoa mwenyewe na nafasi yake akampendekeza Motamma wa Botswana.

Kwa ujumla walioingia wiki hii ni Nando wa Tanzania, Natasha wa Malawi, Oneal wa Botswana, Motamma wa Botswana, Betty wa Ethiopia, Bolt wa Sierra Leon na Elikem wa Ghana.
Tanzania bado ina nafasi nzuri sababu washiriki wote wawili Nando na Feza wapo mjengoni na ndio maana unakila sababu ya kumpigia kura mara nyingi uwezavyo Nando ili aweze kubaki wiki hii. 

Washiriki wawili kati ya saba waliopendekezwa watapita kwenye mlango wa ‘EXIT’ mjengoni hapo Jumapili hii (June 23) wakati wa Eviction Show.

Monday, 17 June 2013

SINTAH AMTOLEA UVIVU OMMY DIMPOZ NA KUMPA LAKE LA ROHONI


Sinta ameandika haya yafuatayo katika website yake:

MDOMO UMEMPONZA HUYU KIJANA

"Daaah masikini akipata matako hulia mbwata, yaani nimesikitishwa na habari ya Ommy Dimpoz na kauli yake aliyotoa kwenye umma, hivi wewe Dimpozi unajua nini cha kuongea ktk public?? SMH usipende kuropoka ropoka tu hata kama wewe ukifa tutajuaje kwenye bank yako kuna kiasi gani acha kuongea kwasababu ya nyimbo tatu ,, Nainai, Badaye na Me n U, Angalia kijana na usiache mbachao kwa msala upitao sasa unajiliza nini katika radio na umeongea mwenyewe hivi hujui mdomo huumba na pia huponza kichwa??

sasa wewe unataka kuniambia u have invested na hutegemei show?? kumbuka sisi mashabiki wako ndio tumekuweka hapo juu na ku support music wako haya tukiacha kupenda nyimbo zako na ukakosa show itakuwaje??? umenizije sasa kumkejeli mwenzio tena kwenye kipaza sauti next time uliza nini cha kuongea ndio maana wenzenu wanakuwa na managers wa kuwa guide sio unaongea tu coz usikike. wenzio walionyamaza uliwaona mafala sio?? au ulitaka utoke kama hivi tukuongeleee cheap cheap fame.

kauli yako uko sahihi ila kwanini usingeiongelea ktk interviews zako kama ushauri kwa wasanii wenzio na ukaifanya ni big issue ktk msiba wa mwenzio??

nimekupa langu la roho kazi kwako sasa ukinichukia sijali, ukinipenda sawa coz naongea ukweli na wananchi waliokerwa wamenituma na sikuwepo ila wamerekodi wakaniambia CEO ifanyie kazi Ommy D katukwaza" says Sintah
Facebook Blogger Plugin by JustNaira.com | Get Widget

ASANTE KWA KUPATA HUDUMA ZETU,TUNAKUOMBA BOFYA LIKE KUUNGANA NASI FACEBOOK

No comments:

Post a Comment

page counter

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Naomba Maoni yako hapa

Scroll to top widget @Netoops Blog.blogspot.com

STEVEN KANUMBA JR AZALIWA, MAMA KANUMBA, MAMA LULU NA LULU WAJAWA NA FURAHA.

Mama Lulu na mama wa marehemu Steven Kanumba wanaonekana kuwa karibu sana siku hizi na hivyo watu kuzidi kuamini kuwa hawana tofauti tena na kusahau yaliyopita. Dada wa marehemu Steven Kanumba amejifungua hivi karibuni katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na mtoto huyo kupewa jina la Steven Kanumba Jr huku mama mzazi wa Elizabeth Michael(Lulu) na mama Kanumba wakiwa na furaha sana, Lulu pia alionyesha furaha yake kwa kuzaliwa mtoto huyo kama picha zinavyoonekana hapo chini. Tunawapongeza tena na tena wazazi hao kwa kuwadhihirishia wanajamii kwa mara nyingine kuwa kila mtu ana amani na mwenzake na hakuna tofauti yoyote kati yao. Mtoto huyo amepewa jina la Kanumba kama ishara ya kumuenzi muigizaji Steven Kanumba aliyekuwa maarufu Afrika mashariki na kuanza kujulikana kimataifa. Angalia picha...........

PICHA YA MTOTO ALIYEZALIWA AKIWA NA MIGUU SITA

Duniani  kuna  mambo....

Huyu  ni  binadamu  mwenzetu  aliyezaliwa  akiwa  na  miguu  sita.Anakaaje,  anasimama vipi.....na  anatembeaje.....Yote tumwachie  mungu  aliyeamua  iwe hivyo